Country Fm Iringa 88.5 Iringa,91.1 Mbeya
Home » » SAMATTA, ULIMWENGU WABEBA TUZO YA KWANZA TP MAZEMBE IKITANGAZWA KIKOSI BORA AFRIKA

SAMATTA, ULIMWENGU WABEBA TUZO YA KWANZA TP MAZEMBE IKITANGAZWA KIKOSI BORA AFRIKA


Kikosi cha TP Mazembe kimeteuliwa kuwa kikosi bora barani Afrika mwaka 2015 katika tuzo za Mwanasoka Bora Afrika zinazoendelea jijini Abuja nchini Nigeria.

Mazembe ambao ni mabingwa watetezi barani Afrika, wametwaa tuzo hiyo na kuwapiga bao USM Alger ya Algeria ambao waliwafunga katika mechi zote mbili za fainali ubingwa wa Afrika.

Watanzania wawili, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wanakipiga katika klabu hiyo ya Lubumbashi, DR Congo.


Katika mechi mbili za fainali, TP Mazembe ilianza kushinda ugenini kwa mabao 2-1, ikarejea nyumbani Lubumbashi na kushinda kwa mabao 2-0.

Katika mechi zote mbili, Mtanzania Samatta alifunga hivyo kuweka rekodi ya kufunga mabao mawili katika mechi mbili za fainali.

Pia katika mechi hizo mbili za fainali, Watanzania hao, Samatta na Ulimwengu, wote walicheza mechi zote mbili, hivyo mchango wao kwa Mazembe kuwa kikosi bora Afrika ni mkubwa sana.
Ahsante kwa maoni yako,endelea kusikiliza redio country fm Iringa-One community
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA COUNTRY FM

Pages

Pages

radio country fm,one community. Powered by Blogger.