Country Fm Iringa 88.5 Iringa,91.1 Mbeya
Home » » Zanzibar wapongezwa uvumilivu wa kisiasa

Zanzibar wapongezwa uvumilivu wa kisiasa


Aidha, kimesema suluhisho la hali ya sasa ya Zanzibar ni vyama vingine vyote, kujumuishwa katika mazungumzo baina ya vyama vya CCM na CUF ili kupata mawazo jumuishi na yatakayowakilisha sehemu kubwa zaidi ya Wazanzibari ambao wengi wao, hasa kizazi kipya, hawana uhusiano wowote na vyama hivyo viwili.
Kauli hiyo imetolewa na Kiongozi Mkuu wa chama hicho, Kabwe Zitto baada ya kikao cha Kamati ya Uongozi iliyokutana Zanzibar mwishoni mwa wiki.
Kwa mujibu wa Zitto, ACT-Wazalendo inasikitishwa na hali ngumu ya maisha inayowakumba wananchi wa Zanzibar kutokana na mkwamo wa kisiasa unaoendelea visiwani humo.
Kutokana na hali hiyo, ACT-Wazalendo imependekeza kwa ajili ya mustakabali mwema wa Zanzibar, mazungumzo yoyote kuhusu uchaguzi uliofutwa yahusishe wadau wa vyama na taasisi nyingine walioshiriki kwenye uchaguzi.
Ahsante kwa maoni yako,endelea kusikiliza redio country fm Iringa-One community
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA COUNTRY FM

Pages

Pages

radio country fm,one community. Powered by Blogger.