Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Paza Mwamlima
Mwamlima alitoa agizo hilo jana wakati wa uzinduzi wa usafi wa
mazingira na upandaji miti uliofanyika eneo la Kituo Kikuu cha Mabasi
yaendayo mikoani Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi.
Alisema yeyote atakayeugua ugonjwa wa kipindupindu wilayani
Mpanda, atapatiwa matibabu, lakini akishapona, atashtakiwa kwa kukiuka
kanuni za usafi.
Mwamlima alisema ugonjwa wa kipindupindu huababishwa na uchafu, hivyo kama mazingira ni masafi, mtu hataugua maradhi hayo.
Aliongeza kuwa wajibu wa kila mtu kuishi kwenye mazingira safi na kuuchukia uchafu ili kuepuka magonjwa ya mlipuko.
Mkuu huyo wa Wilaya amepiga marufuku baa kufunguliwa muda wa kazi
na kucheza bao na watu kushinda kwenye vijiwe vinavyouza kahawa.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Dk. Ibrahim Msengi,
amewaagiza wananchi wa manispaa hiyo kuhakikisha maeneo yao ya kuishi na
wanayofanyia shughuli za biashara yanakuwa katika hali ya usafi.
Alisema kila Jumamosi wananchi wa manispaa hiyo wahakikishe siku hiyo
wanaitumia kufanya usafi kwenye mitaa yao na kwa Jumamosi ya kwanza ya
mwezi, itakuwa inatumika kwa ajiri ya manispaa nzima ya Mpanda.
0 comments:
Post a Comment