WAZIRI KITWANGA ATEMBELEA UHAMIAJI, ATANGAZA OPERESHENI YA KUKAMATA WAHAMIAJI HARAMU NCHINI
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kulia) akimsalimia
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Sylvester Ambokile wakati alipowasili
Makao Makuu ya Uhamiaji, Kurasini jijini Dar es Salaam leo kwa ajili ya
ziara ya kikazi. Wapili kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mbarak
Abdulwakil, na kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, John Mngodo. Katika ziara
hiyo, Waziri Kitwanga aliitaka Idara hiyo ya Uhamiaji kuanz rasmi kwa
operesheni ya kuwakamata Wahamiaji Haramu nchini.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (aliyevaa tai) akiwasalimia
wananchi wanaosubiri kupata huduma ya Hati za Kusafiria katika Ofisi za
Makao Makuu ya Uhamiaji, Kurasini, jijini Dar es Salaam. Waziri
Kitwanga alifanya ziara ya kikazi katika ofisi hizo kwa lengo la
kujifunza kazi mbalimbali zinazofanywa na Uhamiaji. Katika hotuba yake,
licha ya maelekezo mengine aliyoyatoa kwa viongozi wakuu, pia aliitaka
Idara hiyo ya Uhamiaji kuanza rasmi kwa operesheni ya kuwakamata
Wahamiaji Haramu nchini.
Afisa
Uhamiaji anayeshughulika na uchapaji wa Hati za Kusafiria, Amir Hassan
(kushoto), akitoa maelezo ya jinsi wanavyozichapisha Hati za Kusafiria,
kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati)
ambaye alifanya ziara ya kikazi katika ofisi za Makao Makuu ya Uhamiaji,
Kurasini, jijini Dar es Salaam. Kulia ni Kamishna Jenerali wa
Uhamiaji, Sylvester Ambokile.
Kamishna
Jenerali wa Uhamiaji, Sylvester Ambokile (kushoto) akiwa na Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga, wakati Waziri huyo alipokuwa
anafanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya Uhamiaji, Kurasini, jijini Dar
es Salaam kwa lengo la kujifunza shughuli mbalimbali zinazofanywa na
Uhamiaji.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati) akiwaeleza jambo
Watendaji Wakuu wa Idara ya Uhamiaji wakati alipofanya ziara ya kikazi
Makao Makuu ya idara hiyo, Kurasini, jijini Dar es Salaam leo. Wapili
kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak
Abduwakil, na kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, John Mngodo,
na wapili kulia (waliokaa) ni Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Sylvester
Ambokile na kulia ni Kamishna wa Uhamiaji (Utawala na Fedha), Piniel
Mgonja.
Kamishna
Jenerali wa Uhamiaji, Sylvester Ambokile akimfafanulia jambo Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati) wakati Waziri huyo
alipofanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya Uhamiaji, Kurasini, jijini Dar
es Salaam leo.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (wasita kulia), Katibu Mkuu
wa Wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil (watano kushoto), Naibu Katibu Mkuu,
John Mngodo (wanne kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi
Wakuu wa Idara ya Uhamiaji wakati Waziri huyo alipotembelea Makao Makuu
ya Idara ya Uhamiaji, Kurasini, jijini Dar es Salaam. Wasita kushoto ni
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Sylvester Ambokile. Picha zote na
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
NSSF KUKABIDHI DARAJA LA KIGAMBONI JANUARI 2016
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dk. Ramadhani Dau akifafanua jambo.
Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu, Jenista Mhagama akizungumza wakati alipofanya ziara katika Daraja la Kigamboni.
Sehemu ya Daraja la Kigamboni.
Waziri akipata maelezo ya ujenzi wa Daraja la Kigamboni.
Meneja
wa Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Kigamboni, Mhandisi John Msemo
akimuonesha Waziri muunganiko wa barabara zinazoingia katika daraja
hilo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu, Waziri Jenista Mhagama akizungumza na waandishi wa habari.
Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dk. Ramadhani Dau
akitoa ufafanuzi kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge,
Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu, Jenista Mhagama kuhusu
maendeleo ya ujenzi wa Daraja la Kigamboni wakati waziri huyo
alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa daraja hilo, ambapo
ujenzi wake utakamilika mwishoni mwa mwezi Januari mwakani.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu
wenye Ulemavu, Jenista Mhagama (wa pili kushoto) akipata maelezo kutoka
kwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dk.
Ramadhani Dau (katikati) wakati alipofanya ziara ya kuangalia maendeleo
ya ujenzi wa Daraja la Kigamboni jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni
Meneja Mradi ujenzi wa Daraja hilo. Mhandisi Kareem Mataka.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii
(NSSF), Dk. Ramadhani Dau (wa pili kulia), akitoa maelezo kuhusu maendeleo ya
ujenzi wa Daraja la Kigamboni kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,
Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu, Jenista Mhagama (kulia), alipofanya
ziara ya kuangalia maendeleo ya ujenzi wa daraja hilo, ambalo ujenzi wake
utakamilika Januari Mwakani.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,
Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu, Jenista Mhagama (kulia) akipata
maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dk. Ramadhani Dau wakati
alipofanya ziara ya kuangalia maendeleo ya ujenzi wa daraja hilo
ambalo ujenzi wake utakamilika Januari Mwakani.
Na Mwandishi Wetu
WAZIRI wa Sera, Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na
Walemavu, Jenista Mhagama amelitaka Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii
(NSSF), kuhakikisha linakabidhi daraja la Kigamboni ifikapo Januari, 2016.
Pia ametoa fursa kwa shirika hilo na mengine nchini
kama yataweza kuja na mradi wa ujenzi wa daraja kutoka Dar es Salaam hadi
Zanzibar.
Hayo alibainisha jana jijini Dar es Salaam wakati
alipofanya ziara ya kukagua ujenzi wa daraja hilo, ambalo linatarajiwa
kukamilika mwakani.
Alisema ujenzi wa daraja hilo, umegharimu kiasi cha
Dola za Marekani 143.5, ambapo serikali imetoa asilimia 40, huku NSSF ikitoa
asilimia 60 ya fedha zote.
“Tunaliomba shirika hili, lihakikishe linaheshimu nha
kuzingatia muda uliotoa katika kukabidhi daraja hilo mwakani licha ya
kujitokeza ujenzi mwingine wa barabara ya Kilomita moja,”alisema.
Alisema shirika hilo linapaswa kulikabidhi daraja
ifikapo Januari 30 au kabla ya muda huo, kwani ukamilifu wake utapunguza adha
ya foleni na kukuza sekta ya uchumi inayotarajiwa kukuwa kwa kasi.
Katika hatua nyingine, Mhagama alisema endapo mradi
ukiwa katika ubora na viwango vinavyotakiwa utadumu kwa muda mrefu na kuisaidia
Seriali katika kukuza uchumi.
“Miradi ya namna itasaisdia kukuza uchumi wa ndani na
nje ya nchi, pia inatufundisha kujifunza ili kujua kwamba tunaweza kuhimili
miradi mingine mikubwa zaidi ya huu,”alisema.
Kuhusu daraja la kutoka Dar es Salaam hadi Zanzibar,
alisema uwezekano wa kujengwa upo endapo mashirika yakijitokeza na mradi huo. “Kila kitu kinawezekana, hivyo kama Shirika
litajitokeza serikali ipo tayari kwa kila kitu kuunga mkono mkakati watakao
kuja nao,”alisema.
Naye Mkurungenzi wa NNSF, Dk.Ramadhan Dau alisema ujenzi
wa daraja hilo umekuwa wa kasi licha ya matatizo yaliyojitokeza, hivyo
Watanzania watarajie Januari mwakani
kulitumia.
“Bado kuna sehemu nyingine ambazo tutamalizia ila
hadi Januari litakuwa limekamilika kwa asilimia 100, hivyo tunaipongeza serikali
kwa ushirikiano uliotuonyesha,”alisema.
0 comments:
Post a Comment