Maofisa wa polisi
nchini Marekani wanaoshughulika na mapambano ya kuutokomeza ugaidi,
wamesema mkuu wa masuala ya fedha wa kundi la kigaidi la Islamic State
ameuawa kutokana na shambulio la anga karibu na mji wa Tal Afar nchini
Iraq, katika wiki za hivi karibuni.
Ingawa mpaka sasa hakuna taarifa zaidi zilizotolewa kuhusiana na tukio hilo. Vikosi vya kijeshi vya Marekani na vile vya muungano wa majeshi washirika vimekuwa vikiendeleza mashambulizi ya anga dhidi ya wanajeshi wa IS nchini Iraq na Syria kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa.
0 comments:
Post a Comment