MABASI YAENDAYO KASI
MAWAZIRI wawili jana ‘walitumbua majipu’ baada ya kutangaza kusimamishwa kazi kwa Mtendaji Mkuu wa Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka (DART), Asteria Mlambo na Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, Dk Diwani Msemo, wote wakipisha uchunguzi dhidi yao.Mlambo amesimamishwa kazi kuanzia jana ili kupisha uchunguzi baada ya serikali kubaini ukiukwaji wa wazi wa Sheria ya Manunuzi ya Umma katika kumpata mtoa huduma ya mpito wa mradi huo wenye nia ya kupunguza msongamano wa magari barabarani kwa madhumuni ya kurahisisha usafiri na usafirishaji jijini Dar es Salaam.Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, George Simbachawene alisema kutokana na kukamilika kwa sehemu ya ujenzi wa miundombinu ya Awamu ya Kwanza ya mradi, Serikali iliamua kuwa na mtoa huduma wa mpito kabla ya kumpata wa kudumu.“Mtoa huduma wa mpito alipaswa kupatikana kwa mujibu wa Sheria ya Manunuzi ya Umma. Hata hivyo, Serikali imebaini ukiukwaji wa wazi wa sheria hiyo wakati wa kumpata mtoa huduma wa kipindi cha mpito.
“Kufuatia hali hiyo nimeamua kumsimamisha kazi kuanzia leo tarehe 23 Desemba, 2015, Mtendaji Mkuu wa DART, Bi. Asteria Mlambo ili kupisha uchunguzi,” alieleza Simbachawene.
MAWAZIRI wawili jana ‘walitumbua majipu’ baada ya kutangaza kusimamishwa kazi kwa Mtendaji Mkuu wa Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka (DART), Asteria Mlambo na Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, Dk Diwani Msemo, wote wakipisha uchunguzi dhidi yao.Mlambo amesimamishwa kazi kuanzia jana ili kupisha uchunguzi baada ya serikali kubaini ukiukwaji wa wazi wa Sheria ya Manunuzi ya Umma katika kumpata mtoa huduma ya mpito wa mradi huo wenye nia ya kupunguza msongamano wa magari barabarani kwa madhumuni ya kurahisisha usafiri na usafirishaji jijini Dar es Salaam.Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, George Simbachawene alisema kutokana na kukamilika kwa sehemu ya ujenzi wa miundombinu ya Awamu ya Kwanza ya mradi, Serikali iliamua kuwa na mtoa huduma wa mpito kabla ya kumpata wa kudumu.“Mtoa huduma wa mpito alipaswa kupatikana kwa mujibu wa Sheria ya Manunuzi ya Umma. Hata hivyo, Serikali imebaini ukiukwaji wa wazi wa sheria hiyo wakati wa kumpata mtoa huduma wa kipindi cha mpito.
“Kufuatia hali hiyo nimeamua kumsimamisha kazi kuanzia leo tarehe 23 Desemba, 2015, Mtendaji Mkuu wa DART, Bi. Asteria Mlambo ili kupisha uchunguzi,” alieleza Simbachawene.
0 comments:
Post a Comment