Kuna mengi yanaendelea katika soka, tetesi na uvumi katika soka ni moja kati ya vitu vinavyo ingia katika headlines kila siku, vilabu vingi duniani vimekuwa vikijitahidi kuweka usiri katika mambo yake, headlines za kocha wa Manchester United Louis van Gaal kutaka kuachia ngazi klabu hiyo zinazidi kuchukua nafasi.
Jumamosi ya December 5 kocha huyo alikiri kuwa yupo tayari kuondoka Man United
kama wachezaji wa klabu hiyo watapenda aondoke, kwani kumekuwa na uvumi
kuwa wachezaji hawana mahusiano mazuri na kocha huyo, stori zilizotoka
December 7 ni kuwa uongozi wa klabu ya Man United unapanga kumuongezea mkataba, yote hayo yanaandikwa na vyombo vya habari.
Stori ni kuwa kocha wa zamani wa klabu ya Chelsea na Real Madrid muitaliano Carlo Ancelotti amekiri kuvutiwa na kujiunga na Man United
licha ya kuwa hana mpango wa kujiunga na timu yoyote katikati ya msimu,
swali ambalo alijibu mara baada ya kuulizwa kama angependa kuwa kocha
wa Man United.
“Sio
kwamba natafuta klabu iliyo na mipango mikubwa sana kwani naweza
kusubiri kwa sasa sababu sina mpango wa kujiunga na timu katikati ya
msimu, tusubiri hadi mwisho wa msimu kwani nina mipango ya kurudi kazini
msimu ujao. kuhusu kuvutiwa na nafasi ya kuwa kocha wa Man United,
bilashaka hakuna kocha asiyevutiwa na nafasi ya kuwa kocha wa Man
United” >>>> Carlo Ancelotti
0 comments:
Post a Comment