Country Fm Iringa 88.5 Iringa,91.1 Mbeya
Home » » Huyu ndio kocha anayenyemelea kibarua cha Louis van Gaal Man United, kakiri hapa …

Huyu ndio kocha anayenyemelea kibarua cha Louis van Gaal Man United, kakiri hapa …

Kuna mengi yanaendelea katika soka, tetesi na uvumi katika soka ni moja kati ya vitu vinavyo ingia katika headlines kila siku, vilabu vingi duniani vimekuwa vikijitahidi kuweka usiri katika mambo yake, headlines za kocha wa Manchester United Louis van Gaal kutaka kuachia ngazi klabu hiyo zinazidi kuchukua nafasi.

Jumamosi ya December 5 kocha huyo alikiri kuwa yupo tayari kuondoka Man United kama wachezaji wa klabu hiyo watapenda aondoke, kwani kumekuwa na uvumi kuwa wachezaji hawana mahusiano mazuri na kocha huyo, stori zilizotoka December 7 ni kuwa uongozi wa klabu ya Man United unapanga kumuongezea mkataba, yote hayo yanaandikwa na vyombo vya habari.
Stori ni kuwa kocha wa zamani wa klabu ya Chelsea na Real Madrid muitaliano Carlo Ancelotti amekiri kuvutiwa na kujiunga na Man United licha ya kuwa hana mpango wa kujiunga na timu yoyote katikati ya msimu, swali ambalo alijibu mara baada ya kuulizwa kama angependa kuwa kocha wa Man United.
MADRID, SPAIN - JUNE 26:  Carlo Ancelotti holds a press conference after he was presented as Real Madrid's new head coach at Estadio Bernabeu on June 26, 2013 in Madrid, Spain.  (Photo by Denis Doyle/Getty Images)
Carlo Ancelotti
“Sio kwamba natafuta klabu iliyo na mipango mikubwa sana kwani naweza kusubiri kwa sasa sababu sina mpango wa kujiunga na timu katikati ya msimu, tusubiri hadi mwisho wa msimu kwani nina mipango ya kurudi kazini msimu ujao. kuhusu kuvutiwa na nafasi ya kuwa kocha wa Man United, bilashaka hakuna kocha asiyevutiwa na nafasi ya kuwa kocha wa Man United” >>>> Carlo Ancelotti
Ahsante kwa maoni yako,endelea kusikiliza redio country fm Iringa-One community
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA COUNTRY FM

Pages

Pages

radio country fm,one community. Powered by Blogger.