Country Fm Iringa 88.5 Iringa,91.1 Mbeya
Home » »

Hii ndio Top 10 ya wachezaji soka maarufu katika mtandao wa Instagram duniani …

Mtandao wa kijamii wa Instagram umeanzishwa miaka mitano iliyopita ila toka kuanzishwa kwake unatajwa kuwa miongoni mwa mitandao ya kijamii inayokuwa kwa kasi zaidi duniani, huu ndio mtandao ambao maarufu kwa watu kupost picha na video zao. December 10 mtu wangu naomba nikusogezee Top 10 ya mastaa maarufu zaidi katika mtandao wa Instagram yaani wanafollowers wengi.
Cristiano Ronaldo ambaye ni mkali wa kuvunja rekodi za soka kwa sasa ndio staa wa soka anayetajwa kuwa na wafuasi wengi katika mitandao yote ya kijamii. Huenda ukawa unashangazwa na list ya wachezaji wa America kuwa wengi katika list hii, ukweli ni kwamba America mtandao wa Instagram unatajwa kuwa na watumiaji milioni 400 na milioni 39.5 kati ya hao wamewafollow wachezaji soka wakubwa. Hii ndio Top 10 mtu wangu.
10- Thiago Silva wa klabu ya Paris Saint Germain ya Ufaransa (PSG) ana followers milioni 8
62838
Thiago Silva
9- Karim Benzema wa klabu ya Real Madrid ya Hispania na timu ya taifa ya Ufaransa ana followers milioni  8.3
Benzema6-1024x1024
Karim Benzema
8-Ronaldinho ambaye aliwahi kuchezea timu ya taifa ya Brazil ila kwa sasa hana timu ana jumla ya followers milioni 8.7 .
Dinho-1024x1024
Ronaldinho
7- Zlatan Ibrahimovic mshambuliaji wa klabu ya PSG ya Ufaransa na timu ya taifa ya Sweden ana followers milioni 10.
zLATAN
Zlatan Ibrahimovic
6- David Luiz listi hii wachezaji wa Paris Saint Germain (PSG) ya Ufaransa wametawala, yeye ana followers milioni 11.
dAVID
David Luiz
5- Gareth Bale ni mchezaji anayeshikilia rekodi ya usajili ya Dunia anaitumikia klabu ya Real Madrid ya Hispania na timu ya taifa ya Wales ana jumla ya followers milioni 11.4
Bale11
Gareth Bale
4- James Rodriguez anakipiga katika klabu ya Real Madrid anatajwa kufikia followers milioni 16.7
R2-1024x999
James Rodriguez
3- Lionel Messi wa FC Barcelona na timu ya taifa ya Argentina anatajwa kuwa na followers milioni 30.5
Messi-g
Lionel Messi
2- Neymar ndio mchezaji wa pili wa FC Barcelona kuwa katika hii list ana followers milioni 36.5
Neymar-vg
Neymar
1- Cristiano Ronaldo wa Real Madrid ndio anatajwa kuwa staa maarufu zaidi katika mitandao ya kijamii ikiwemo instagram ana followers milioni  39.4
Ronaldo34-1024x1024
Cristiano Ronaldo
Ahsante kwa maoni yako,endelea kusikiliza redio country fm Iringa-One community
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA COUNTRY FM

Pages

Pages

radio country fm,one community. Powered by Blogger.