Country Fm Iringa 88.5 Iringa,91.1 Mbeya
Home » » HAWA NDIYO WACHEZAJI WA CHELSEA WANAOCHEZA CHINI YA KIWANGO KWA MANENO YA Jose Mourinho

HAWA NDIYO WACHEZAJI WA CHELSEA WANAOCHEZA CHINI YA KIWANGO KWA MANENO YA Jose Mourinho

Image result for MOURHINO
 Klabu ya soka ya Chelsea ambayo inashuka dimbani December 14 kucheza mchezo wake wa 16 wa Ligi Kuu Uingereza msimu wa 2015/2016 dhidi ya klabu ya Leicester City. Chelsea inaenda kucheza mchezo huo ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza mechi 8 msimu huu katika mechi zake 15 za Ligi ambazo tayari imecheza.
WEST BROMWICH, ENGLAND - AUGUST 23: Referee Mark Clattenburg shows the red card to John Terry of Chelsea during the Barclays Premier League match between West Bromwich Albion and Chelsea at The Hawthorns on August 23, 2015 in West Bromwich, England. (Photo by Michael Regan/Getty Images)
Mara kadhaa kocha wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho amekiri kuwa, moja kati ya vitu vinavyochangia kikosi chake kufanya vibaya ni wachezaji kucheza chini ya kiwango, baada ya kuongea maneno hayo mara kadhaa, December 13 Jose Mourinho amewataja wachezaji wake wanne ambao anafikiri hawako katika kiwango chao kama msimu uliyopita.
Chelsea's Branislav Ivanovic, left, and Swansea's Jefferson Montero challenge for the ball during the English Premier League soccer match between Chelsea and Swansea City at Stamford Bridge stadium in London, Saturday, Aug. 8, 2015. (AP Photo/Frank Augstein)
“Kama utaangalia uwezo wa mchezaji mmoja mmoja utaona kuwa Branislav Ivanovic, Gary Cahill, John Terry msimu uliyopita walikuwa na uwezo mzuri sana, lakini huu msimu ni ngumu kusema mchezaji fulani yuko vizuri, uwezo wao karibu wote ni sawa, sioni utofauti wa Cesc Fabregas na wala sioni akiogopa kukaa na mpira wala kufanya makosa” >>>  Jose Mourinho
Cesc-Fabrigas
Klabu ya Chelsea wiki iliyopita ilipoteza mchezo wake wa nane wa Ligi Kuu Uingereza katika dimba lake la nyumbani Stamford Bridge dhidi ya timu iliyopanda daraja msimu huu Bournemouth, licha ya kutwaa Ubingwa msimu uliyopita, Chelsea pamoja na kocha wao Jose Mourinho wapo katika wakati mgumu msimu huu.
Ahsante kwa maoni yako,endelea kusikiliza redio country fm Iringa-One community
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA COUNTRY FM

Pages

Pages

radio country fm,one community. Powered by Blogger.