Country Fm Iringa 88.5 Iringa,91.1 Mbeya
Home » » Serikali imetakiwa kusimamia sheria ya mizani na vipimo ya mwaka 1982

Serikali imetakiwa kusimamia sheria ya mizani na vipimo ya mwaka 1982



IRINGA
Serikali imetakiwa kusimamia sheria ya mizani na vipimo ya mwaka 1982kwa umakini  ili wakulima na wafanyabiashara waweze kunufaika na kilimo.

Ushauri huo umetolewa na mwenyekiti wa chemba ya wafanyabiashara mkoani Iringa TCCIA Bw Lukas Mwakabungu wakatika akiongea na kituo hiki.
Bw Mwakabungu amesema ili usimamizi huo ufanyike kwa ufanisi ni vyema viongozi wote wakawajibia kuanzia  katika ngazi ya juu ya uongozi wakiwemo wakuu wa mikoa.
Aidha mwakabungu amesema halmashauri za wilaya zinatakiwa kuunda sheria ndogondogo zitakazo wabana wakiukaji wa sheria ya mizani na vipimo ya mwaka 1982.
Hata hivyo amewataka wafanyabiashara kufanya kazi kwa kuzingatia sheria za nchi na kutokukwepa kulipa kodi kwani kukwepa kulipa kodi ni kuikosesha serikali kupata mapato yake halisi.
MWISHO
Ahsante kwa maoni yako,endelea kusikiliza redio country fm Iringa-One community
Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Joseph Kipangula Enhanced by Joseph Kipangula

0 comments:

Post a Comment

SIKILIZA COUNTRY FM

Pages

Pages

radio country fm,one community. Powered by Blogger.